Madaktari bingwa nchini Kenya wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kuwatenganisha pacha wawili
Madaktari bingwa nchini Kenya wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kuwatenganisha pacha wawili
Madaktari bingwa nchini Kenya wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kuwatenganisha pacha wawili walioungana katika sehemu ya chini ya mgongo.
Pacha hao walikuwa hospitalini kwa muda wa miaka miwili tangu walipozaliwa wakingoja upasuaji wa kuwatenganishwa.
Walizaliwa
mwaka wa 2014 wakiwa na viungo vyote vya mwili isipokuwa sehemu ya
chini ya uti wa mgongo ulioshikana na kuwasababisha kutumia njia moja
kuenda haja kubwa.
Upasuaji wa aina hiyo kutenganisha sehemu ya uti wa mgongo ndio wa kwanza kufanyika katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara.
Post a Comment