Mkwasa aita 24 KUCHEZEA 2016Taifa Stars
Mkwasa aita 24 KUCHEZEA 2016Taifa Stars
Kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Charles Boniface Mkwasa ametaja kikosi cha wachezaji 24 kitakachoingia kambini Novemba saba kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Zimbabwe utakaopigwa Novemba 13 mwaka huu nchini humo.
Nyota wa Stars walioitwa na Mkwasa ni:
Makipa
Deogratius Munishi –Young Africans
Said Kipao –JKT Ruvu
Aishi Manula –Azam FC
Mabeki
Erasto Nyoni -Azam FC
Michael Aidan -JKT Ruvu
Mwinyi Haji -Young Africans
Mohamed Hussein –Simba SC
David Mwantika -Azam FC
James Josephat –Tanzania Prisons
Vicent Andrew -Young Africans
Viungo wa Kati
Himid Mao -Azam FC
Mohammed Ibrahim –Simba SC
Jonas Mkude –Simba SC
Muzamiru Yassin –Simba SC
Viungo wa Pembeni
Abdulrahman Mussa -Ruvu Shooting
Shiza Kichuy –Simba SC
Simon Msuva -Young Africans
Jamal Mnyate –Simba
Washambuliaji
Ibrahim Ajib –Simba SC
John Bocco -Azam FC
Mbwana Samatta -K.R.C Genk ya Ubelgiji
Elius Maguli –Oman
Thomas Ulimwengu –Mchezaji huru
Omar Mponda -Ndanda
Kwa sababu mbalimbali hususani majeruhi, Mkwasa amewaacha wachezaji Shomari Kapombe (Azam FC), Hassan Kabunda (Mwadui FC), Juma Abdul na Juma Mahadhi wa Young Africans.
Mchezo huo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika jijini Harare, umeratibiwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo huwa na kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa kwa wanachama wake – Tanzania ni miongoni mwao. Shirikisho la Mpira wa Miguu la Zimbamwe liliomba TFF mchezo huo.
Matokeo ya mchezo huo, ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 144 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Zimbambwe yenyewe inashika nafasi ya 110.
Post a Comment