YANGA KUSAJILI KOCHA MPYA
YANGA KUSAJILI KOCHA MPYA
KOCHA mpya wa Yanga,
Mzambia George Lwandamina anatarajiwa kutua nchini Jumatano baada ya kumalizana
na klabu yake ya sasa, Zesco United ya kwao
Justin Mumba na Katebe
Chengo Mtendaji Mkuu wa ZESCO na Ofisa Habari wametoa taarifa ya kuachana na
Lwandamina.
Lwandamina ambaye
amekwishamalizana na uongozi wa Yanga jana aliiongoza Zesco United katika mechi
ya Ligi Kuu ya Zambia dhidi ya Nkana FC na leo anatarajiwa kuwa na kikao na
waajiri wake.
Uongozi wa Yanga unataka kumuondoa kocha Hans
van der Pluijm na Wasaidizi wake wote, Juma Mwambusi, kocha wa makipa Juma
Pondamali na Meneja Hafidh Saleh wote wazalendo na kuwaleta Mzambia Lwandamina
atakayekuwa Kocha Mkuu, akisaidiwa na wazalendo Charles Boniface Mkwasa,
Manyika Peter kocha wa makipa na Meneja, Sekilojo Chambua.
Hata hivyo, mpango huo unakabiliwa na upinzani
mkali kutoka kwa wadau wa timu hiyo na wapenzi wanaoamini Pluijm bao chaguo
sahihi Jangwani.
Ikumbukwe wiki mbili zilizopita Pluijm alisusa
kwa siku tatu kufanya kazi Yanga na kuwasilisha barua ya kujiuzulu baada ya
kukerwa na taarifa za ujio wa Lwandamina.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba
aliingilia kati suala hilo na kufanikiwa kumrejesha kazini Pluijm.
Waziri Mwigulu ambaye ni mpenzi na mwanachama
wa Yanga, kwanza aliushauri uongozi kumrudisha Pluijm na baadaye akaenda
kuzungumza na kocha huyo pia kumshauri akubali kurejea.
Baadaye akazikutanisha pande zote mbili,
Pluijm na uongozi wa Yanga katika kikao ambacho inaelezwa makubaliano
yalifikiwa kabla ya uongozi wa Yanga kumemuandikia barua Mholanzi huyo kumuomba
radhi.
Post a Comment